Biblia: Kitabu kutoka kwa Mungu



Kuna maswali mengi unaweza kujiuliza Biblia inatofautianaje na vitabu vingine? 

Biblia inawezaje kukusaidia kukabiliana na matatizo yako? Kwanini unaweza kuamini unabii mbalimbali ulio katika Biblia? 

Hebu wazia jinsi ulivyohisi ulipopata zawadi ya pekee kutoka kwa rafiki yako. Haikosi ulisisimuka na kufurahi kwelikweli. Mtu anapokupa zawadi anaonyesha kwamba anakuthamini. Bila shaka, ulimshukuru rafiki yako kwasababu ya zawadi hiyo. 

Biblia ni zawadi kutoka kwa Mungu, nasi tunapaswa kuithamini kwelikweli. Kitabu hicho ni cha pekee hufunua mambo ambayo tusingeweza kuyajua kwa njia niyingine yoyote. Kwa mfano, Biblia inatuambia kuhusu kuumbwa kwa mbingu zenye nyota, dunia hali kadhalika mwanaume na mwanamke wa kwanza. 

Biblia ina kanuni zenye kutegemeka zinazotusaidia kukabilia na matatizo na mahangaiko ya maisha. Inaeleza jinsi Mungu atakavyotimiza kusudi lake na kuleta hali bora duniani. Biblia ni zawadi nzuri kama nini! Pia Biblia ni zawadi inayochangamsha moyo kwa sababu inatueleza jambo fulani kumhusu Mpaji mwenyewe  Mungu. 

Kwa kuwa ametupa Biblia ni wazi kwamba anataka tumjue vizuri. Kwa kweli, Biblia inaweza kukusaidia kumkaribia Mungu. Katika nyakati za sasa Watu wengi wana Biblia. 

Biblia imechapishwa katika lugha zaidi ya 2,300 ikiwa nzima au sehemu na kwa hiyo zaidi ya asilimia 90 ulimwenguni wanaweza kuipata. Kwa hakika hakuna kitabu kingine kilicho kama Biblia. Isitoshe Biblia imeongozwa na roho ya Mungu (2 Timotheo 3:16) Jinsi gani? Biblia yenyewe inajibu, “Wanadamu walisema yaliyotoka kwa Mungu kama walivyoongozwa na roho takatifu.” Pia kitabu cha 2 Petro 1:21; 

Kwa mfano, huenda babu akamwomba mjukuu wake amwandikie barua. Mjukuu huyo ataandika mawazo na maagizo ya Babu huyo. Kwa hiyo barua hiyo ni ya babu huyo wala siyo ya mjukuu wake. 

Vivyo hivyo Biblia ina ujumbe wa Mungu wala si wa watu waliotumiwa kuiandika. Kwa hiyo Biblia kwa kweli ni “Neno la Mungu.” – 1 Wathesalonike 2:13 Biblia iliandikwa zaidi ya miaka 1,600. Walioiandika walikuwa watu wa hali mbalimbali walioishi nyakati tofauti . 

Baadhi yao walikuwa wakulima, wavuvi, na wachungaji. Wengine walikuwa manabii, waamuzi na wafalme. Luka aliyeandika Injili alikuwa dakitari. 

Licha ya malezi mbalimbali ya watu walioiandika, Biblia ina upatano tangu mwanzo mpaka mwisho. Hivyo basi sio zawadi pekee bali ni sahihi na ina upatano.

Imetayarishwa na Jabir Johnson……………..Oktoba 13, 2019.  

Post a Comment

0 Comments