Mimea na Matunda ina ulazima katika makuzi ya kiroho?


Sisi sote tunayo mahitaji halisi. Makubwa kati ya hayo ni haya: upendo, usalama na umuhimu. 

Ndani ya mahitaji hayo, tunayo mahitaji mengine yaliyo wazi zaidi. Baadhi ya watu wanahitaji chakula na mavazi, wengine wanahitaji watoto wao wamjue Mungu, wengine wanahitaji kuponywa magonjwa, na mahitaji mengine kadha wa kadha. 

Matumizi ya mimea na matunda yanapunguza ukatili dhidi ya wanyama ambao kwa kiasi kikubwa wamekuwa wakichinjwa kila siku kwa ajili ya vitoweo na wakati mwingine wanyama hawa wametumika katika bidhaa mbalimbali. 

Wanaotumia mimea na matunda wamejiepusha kwa kiasi kikubwa na matumizi hayo kwa kwenda mbali zaidi kuacha kabisa kutumia mazao mengine yanayotokana na wanyama na ndege hao kama vile nyama, mayai, na asali pia matumizi ya ngozi. 

Hata hivyo vegetarians wanaamini kuwa kuacha kutumia vitu hivyo ni mojawapo ya njia ya kuwaokoa wanyama hao, pia kutunza mazingira na kutunza afya zao wenyewe. 

Tafiti mbalimbali za wanasayansi zinaonyesha matumizi ya nyama ambayo ndani yake ina mafuta na protini ni chanzo kikubwa cha magonjwa ya moyo, kansa ya mapafu na utumbo, kisukari, Unene wa kupitiliza. 

Hatuwezi kuziweka pembeni juhudi za Hom Jay Dinshah (1993-2000) ambaye alipambana kusambaza elimu kuhusu matumizi ya mimea na matunda kipindi chote cha uhai wake kupitia Jarida la Ahimsa (1960-2000). 

Dinshah aliweka bayana mchango wa wakongwe Mahtma Gandhi na Albert Schweitzer kama mhimili mkubwa wa AHIMSA katika kitabu chake cha ‘Out of Jungle.’ Dinshah alizaliwa Novemba 2, 1933 na kufariki dunia Juni 8, 2000 akiwa na umri wa miaka 66 kwa mshtuko wa moyo.

Imetayarishwa na Jabir Johnson……………………….Oktoba 31, 2019

Post a Comment

0 Comments