Unaikumbuka miaka 75 ya kuanzishwa TAG

Tanzania Assemblies of God (TAG) ni Kanisa lililotokana na uamsho mkubwa ulioanza huko mtaa wa AZUSA, California (Marekani), mwanzoni mwa karne ya 20.

Deer ambaye awali alikuja kama Mmisionary wa kujitegemea, na alianzisha Kanisa la Pentecoste Holiness Association (PHA) mnamo mwaka 1928 ambapo ibada ya kwanza hasa ya Kanisa hilo lilianza mapema mwaka 1929 huko Igale, Mkoa wa Mbeya.

Mnamo mwaka 1938 Paul Derr alirejea Marekani na mwaka uliofuata 1939 alijiunga na Kanisa la Assemblies of God, na hivyo kuikabidhi kazi iliyokuwa imeanzishwa Tanzania (wakati huo ikiitwa Tanganyika) mikononi mwa Genenral Council ya Assemblies of God Marekani. Na kuuomba uongozi huo wampeleke Mmissionari kwenye kazi hiyo kuilea wakati yeye akiwa likizoni.   

Historia inatuonesha kuwa katika miaka ya mwanzo  kanisa lilisimamiwa  wamishenari wa  kimarekani, wachungaji wa kiafrika  wakati huo, Yohana Mpayo (Marehemu) na  Petros, walikuwa maaskofu  chini ya Assemblies of God Mission.

Kanisa liliendelea kuongozwa katika mfumo huo hadi mwaka 1967. Kanisa la kwanza kabisa la TAG lilikuwapo pale Igale, Wilaya ya Mbalizi, Mkoa wa Mbeya.

Ni mwaka huo wa 1967, uongozi wa Assemblies of God Mission, uliamua kulikabidhi kanisa kwa uongozi wa wenyeji na Mchungaji Immanuel Lazaro, alichaguliwa kuwa Askofu Mkuu wa kwanza mtanzania wa  kuongza Tanzania Assemblies of God (TAG).

Kanisa hili liiingia hapa nchini kama matokeo ya uamsho mkubwa wa Kipentekoste uliotokea kule Azuza Marekani.

Hivyo malengo makuu ya kuanzishwa kwa kanisa ni kuwafikia wenye dhambi kwa injili iliyo hai, iletayo wokovu na kuleta uamsho mkubwa wa Bwana wetu Yesu Kristo nchini Tanzania.


Ili kutimiza malengo hayo ilikuwa lazima watendakazi shambani mwa Bwana waandaliwe tangu utoto wao.


Post a Comment

0 Comments