Tuliumbwa tuishi milele?


Ni nani kati yetu asiyetamani kuishi maisha marefu yaliyojaa furaha? Wazia jinsi ambavyo maisha yangekuwa ikiwa tungeishi milele tukiwa na afya kamili na furaha!

Tungekuwa na nafasi ya kutosha ya kushirikiana na wapendwa wetu, kutembelea sehemu mbalimbali duniani, kujifunza fani tofauti-tofauti, kuwa na hekima zaidi na kujifunza kwa kina jambo lolote linalotuvutia mpaka tunapohisi tumeridhika.

Je ni vibaya kutamani maisha kama hayo? La hasha! 

Mungu hakukusudia wanadamu wawe wakifa. Wazazi wetu wa kwanza, Adamu na Hawa, waliumbwa bila kasoro yoyote kwenye mwili na akili; wangekuwa hai hadi leo. 

Maneno ambayo Mungu alimwambia Adamu kuhusu mti Fulani uliokuwa kwenye bustani ya Edeni yanathibitisha hilo.


 “Walakini matunda ya mti wa ujuzi wa mema na mabaya usile, kwa maana siku utakapokula matunda ya mti huo utakufa hakika.” Mwanzo 2:17

Post a Comment

0 Comments