WAKRISTO WATAKIWA KUISHI MAISHA YA UVUMILIVU KAMA DAUDI

Uvumilivu, kukaa kimya wakati wa changamoto za maisha, kuheshimu uongozi uliopo na kujua kuwa ahadi za Mungu kwa mtu wake zitatimilika kwa wakati wake ni mambo ya msingi katika maisha ya Mkristo.
 MCHUNGAJI VINAC AMNON MWAKITALU

Akihubiri katika Ibada ya Jumapili Mchungaji na Mwalimu Vinac Amnon Mwakitalu wa Kanisa la Tanzania Assemblies of God Ilomba Mbeya alisema hizo zilikuwa kanuni za msingi katika maisha ya Mfalme Daudi kabla ya kukalia kiti hicho na hata baada ya kuingia madarakani.

Mchungaji Mwakitalu alisema mwamini anapaswa kuwa mvumulivu na mwenye subira pindi apitiapo changamoto mbalimbali za kimaisha kubwa zaidi kukaa kimya na kumsubiri Mungu atende kwa wakati wake.

Aliongeza kusema wakristo wamefikia hatua mbaya pindi waingiapo kwenye changamoto za kimasiha kujikuta wakimwacha Mungu huku wakiendelea kuingia katika majumba ya Ibada hali ambayo ameiita kuwa ni kupoteza muda.

Mchungaji Mwakitalu aliongeza kusema Daudi alipotenda dhambi alitubu mara moja kwani ndani yake alikuwa na Roho wa Mungu, na kwamba hata siku za leo kwa mtu aliyejaa Roho Mtakatifu  hawezi kukaa kimya akisha tenda dhambi.

Hata hivyo Mchungaji Mwakitalu aliwataka waumini wa kanisa hilo kwa ujumla wake kuwa waombaji ili kuendelea kutunza ushirika na Mungu na kuwa wa kipekee katika jamii.

Aidha Mchungaji Mwakitalu aliweka bayana maisha ya Daudi ya kujali Ibada na kazi ya Mungu kwa ujumla.

Johnson Jabir
            Januari 23, 2012

Post a Comment

0 Comments