Theolojia: Uumbaji wa Mungu mpaka Gharika


Mbingu na dunia zilitoka wapi? Jua, mwezi na nyota na vitu vingi duniani vilitokea namna gani? Biblia inatoa jibu la kweli inaposema viliumbwa na Mungu. 


Basi hapo tunajifunza kwamba watu wa roho ndio walioumbwa kwanza na Mungu, wakawa kidogo kama yeye . Hao ni malaika. Lakini dunia iliumbwa kwa ajili ya watu kama sisi. 


Halafu Mungu akaumba mwanaume na mwanamke walioitwa  Adamu na Hawa (Eva), kisha akawaweka katika bustani nzuri. Lakini hawakumtii Mungu, wakaipoteza haki ya kuendelea kuishi.

Jumla ya miaka kutoka kuumbwa Adamu mpaka Gaharika Kuu ni 1656. 

Wakati huo waliishi watu wengi wabaya. Huko mbinguni, walikuwako watu wa roho wasioonekana, Shetani na malaika zake wabaya. Hapa duniani walikuwako Kaini na watu wengine wabaya na watu wakubwa mno. 

Lakini walikuwako pia watu watu wazuri duniani Habili, Henoko na Nuhu. 

Mtayarishaji: Jabir Johnson

Post a Comment

0 Comments