Historia ya Ukristo-1



UTANGULIZI
Kitabu cha “Historia ya Ukristo” kilichoandikwa na Deam A. Peterson na kuchapishwa na Central Tanganyika Press, mwaka 1969 kinaeleza mengi kuhusu historia ya ukristo lakini kubwa zaidi katika kitabu hicho anaeleza kuwa sio watoaji wote na kila chuo cha theolojia hukubaliana na mafundisho yote yaliyomo. Peterson ameangazia maeneo mbalimbali kama ifuatavyo;
  • Hali ya Ulimwengu mwanzoni mwa Kanisa
  • Kuenea na kuteswa kwake Kanisa
  • Maendeleo na mabishano ya Theolojia
  • Umoja na Utawala wa Kanisa
  • Majadiliano ya Theolojia zamani za Mfalme Konstantino.
  • Umonaki wa Kikristo
  • Kanisa wakati wa ushindi wa mataifa makorofi ya Ulaya.
  • Upapa wa Rumi na uenezi wa Injili
  • Kanisa la Mashariki zamani za A.D 500-1000.
  • Kanisa la Magharibi     
Nami sitatofautiana sana na Peterson, nitaendelea kupita humo humo katika kuendelea kutunza historia hiyo na kuongeza baadhi ya mambo kutokana na wakati tulio nao kutoka vyanzo mbalimbali.

Maneno ya Dean A. Peterson
Historia ya Kanisa la Kikristo yaweza kuandikwa kwa kufuata mipango mbalimbali. Yawezekana iandikwe kueleza jinsi kanisa lilivyoenea kutoka Yerusalemu hata pande zote za dunia. Yawezakana historia ya kanisa iandikwe kwa kufuata mikazo na mabishano ya theolojia, kwani hayo yamo sana katika maisha yake. Tena inawezekana tuchunguze maisha ya watu mashuhuri waliotenda makuu katika historia ya kanisa. Njia hizo, pamoja na njia nyinginezo , huwa na faida yao. Mwandishi wa kitabu hiki (Historia ya Ukristo), amevutwa kushirikisha njia hizo tatu akijaribu kuonyesha historia ya kanisa kwa kufuata makuu ya uenezi wake nay a theolojia yake kwa njia ya kuyachungulia maisha ya watu wake. Historia ya kanisa ni habari za maisha ya watu, wakuu kwa wadogo. Katika kuona jinsi walivyopatwa na nguvu ya Mungu katika Kristo tutapokea baraka kwa maisha yetu ya leo. Tenakwa kuchunguza jinsi walivyoshindania maisha ya kikristo katika mazingira katika mazingira yao tutapewa uongozi na hekima zihitajiwazo katika ulimwengu wa leo. Ujuzi wote haumo katika kizazi chetu. Kukataa mafundisho ya karne zilizopita ndiko kujiweka katika umaskini wa ujinga. Haya basi, tuanze kutazama habari za mababa zetu katika Imani. Najua kwamba kitabu hiki kingefaa zaidi kama kingeandikwa na Mwafrika. Maana usemi wake na mikazo yake ingelenga shabaha sawasawa. Lakini kwa kuwa huyo hajapatikana kwa kazi hii mpaka sasa, najaribu niwezavyo nikitumaini ya kuwa kitabu hiki kitaleta msaada mpaka kingine kifaacho zaidi kitatolewa.”

Shabaha kubwa ya kukuletea masuala haya ni pamoja na kujaribu kutunza kumbukumbu kwa njia ambazo zinaweza kuwa msaada kwa vizazi vijavyo. Kama ambavyo wao walipambana kutunza kwa njia ya kuandika kwenye vitabu kwa karne ya 21 tunapambana kutunza katika mtandao wa Intaneti ili watakaokuja baada yetu au wanaotaka kujua kuhusu ukristo waweze kupata rejea mbalimbali ambazo zitaweza kuwasaidia kupata mambo yaliyopita.

Historia ya Kanisa ambayo nitaanza kuiweka hapa itakuwa katika maeneo makuu matatu ambao ni Historia ya Kanisa la karne ya kwanza hadi kumi, Historia ya Matengenezo (Reformation) karne ya 11 hadi 17 na Historia ya Kanisa katika karne ya 18 hadi 20.


HALI YA ULIMWENGU MWANZONI MWA KANISA
Hapa kuna vipengele vingi vya kuangalia kama vile Utawala wa Warumi, Elimu ya Wayunani, Wayahudi wa wakati huo, Yesu Kristo na kanisa lake.

Post a Comment

0 Comments