KONGAMANO LA PASAKA KWA VYUO VIKUU MBEYA -THE OPEN UNIVERSITY OF TANZANIA MBEYA CAMPUS


U
ongozi wa Ushirika wa Kikristo wa Wanavyuo Tanzania(USCF) mkoa wa Mbeya unatarajia kufanya Kongamano la Pasaka litakalofanyika katika Ukumbi wa Chuo Kikuu Huria Tanzania Kampasi ya Mbeya.
Mwenyekiti wa USCF Mbeya Peniel Sarakikya amesema Kongamano hilo lenye Kauli Mbiu KUENENDA KATIKA ROHO litaanza Aprili 6 hadi 8 mwaka huu.

Sarakikya ameongeza kusema kiingilio kitakuwa Shilingi 10,000/= za Tanzania ambapo ndani yake kwa wale waliotoa watakuwa wakipata chakula cha mchana.

Pia Mwenyekiti huyo amewataja watumishi wa Bwana watakao fundisha katika Kongamano hilo ni Mchungaji Nguvila, Mchungaji Oscar, Mchungaji Prince Mollel, Mchungaji Mariam Kyomo, Mchungaji Erick, Mwalimu George Makoja na Mtume  Paul Njoroge.

CHANZO: USCF Mbeya

Post a Comment

0 Comments