WANAFUNZI WA VYUO VIKUU WATAKIWA KULISHIKA NENO LA MUNGU

WANAFUNZI wa Vyuo Vikuu mkoani Mbeya wametakiwa kulishika Neno la Mungu ili wamuone Mungu katika maisha yao wawapo masomo.
 MWALIMU GEORGE MAKOJA AKIFUNDISHA
Akifundisha katika Kongamano la Pasaka kwa wanafunzi hao lililofanyika katika katika ukumbi wa Mbeya Sekondari Jijini Mbeya; Mwalimu George Makoja alisema Shetani amekuwa mjanja sana tangu kuumbwa kwa ulimwengu ili kumrudisha mwanadamu nyuma asijua uzuri wa Mungu Mwenyezi.

Mwalimu George alisema kuwa Neno la Mungu ni chanzo cha mafanikio ya kiroho, kimwili hata nafsi hivyo kulishika kwa umakini mkubwa ni jambo la muhimu sana.

Hata hivyo alinukuru maandiko kutoka Biblia kwenye vitabu vifuatavyo kutioa uzito; Luka 4:1-; Yoshua 1;8.

Aidha alisema kuwa katika vyuo vikuu  kumwemwagwa mapepo kwa ajili ya kuteketeza kundi hili la vijana na kwamba ili kujilinda Neno ala Mungu ndilo Jibu.

Walimu katika Kongamano hilo la USCF walikuwa Mchungaji Nguvila, Mchungaji Oscar, Mchungaji Prince Mollel, Mchungaji Mariam Kyomo, Mchungaji Erick, Mwalimu George Makoja na Mtume  Paul Njoroge.

Kongamano la USCF limehitimisha jana Aprili 8, 2012.

Post a Comment

0 Comments