MARIA NKWAMA: SHIKA NENO KWA FAIDA YA VIZAZI VIJAVYO

MAISHA YALIYO NA NIDHAMU HUWA YA FURAHA NA HEKIMA” ndivyo ambavyo Mwalimu wa Shule ya Uanafunzi wa Darasa la Mabalozi wa Yesu (C.A’s) wa Kanisa la Tanzania Assemblies of God Ilomba Mbeya alivyaoanza kufundisha.
Katika darasa hilo Mwalimu Maria Nkwama alifundisha somo kuhusu Hekima ya Nidhamu na kuiweka katika makundi mawili ambayo ni Maonyo yatolewayo na Mzazi kwa Mtoto na Maonyo yatolewa na Mwenyezi Mungu kwa watendao dhambi.

Akifundisha kwa msisitizo Mwalimu Maria Nkwama aliwaasa wanafunzi hao kulishika Neno la Mungu kwani sio kwa faida ya sasa pekee bali hata kwa vizazi vijavyo.

Pia aliongeza kuwa hakuna mtu kwa asili ambaye alizaliwa akiwa na tabia njema hivyo kumfanya awe mzuri ni lazima  atengenezwe kwa mafundisho ya Neno la Mungu.

Post a Comment

0 Comments