Kanisa latakiwa kutenga muda wa kutosha kumjua Mungu



6 Julai 2014
Jumapili
Venue: Amani Cathedral Centre
Soweto, Moshi-Kilimanjaro.
Mhubiri: Mama Mchungaji Benjamin Bukuku
Sura Kuu: 1 Nyak. 28:9
Kichwa: KUMJUA MUNGU

MAMA MCHUNGAJI BENJAMIN BUKUKU


Katika ibada hiyo iliyokuwa na watau zaidi ya 200, Mtumishi wa Bwana alianza kwa kusema Kumjua Mungu, sio kazi nyepesi. Inahitaji muda wa kutosha nah ii ndio sababu ya waumni kutakiwa kuwemo hekaluni mwa Bwana, kila kukuchapo.
Daudi aliona vema, kumrithisha mtoto wake, Mungu aliyezifanya Mbingu na nchi. Daudi alijua wazi  kwamba mali za dunia hii haziwezi kumsaidia sana Suleiman bali kumfahamu Mungu ndio kila kitu.
Usipomjua Mungu kiundani utateswa na kila uchafu wa dunia hii. Kumetokea imani nyingi zinazodai kuwa zinamhuburi Mungu Aliye juu, lakini ukizichunguza sana utagundua imani hizo hazina chochote zaidi ya kuwatesa binadamu.
Zab:23 1. BWANA ndiye mchungaji wangu,
                 Sitapungukiwa na kitu….
Bwana Mungu anapaswa kuwa mchungaji wa maisha yako siku zote za maisha yako hapa ulimwenguni.
1 Sam. 16:1-
Unamjua Mungu wako, ni wa namna gani? Hapa kuna alama ya msingi…. “Naked eye” (macho ya nyama). Macho ya nyama yanweza kukupa matokeo tofauti (wakati mwingine) sio mara zote yatatoa jawabu sahihi.
Huwezi kumjua Mungu kirahisi, kama husomi Neno lake kwani huko ndiko kwenye siri ya mafanikio.
1 Sam. 17:22-
Ukimtafuta , ataonekana bila shaka. Ukimjua Mungu utafanya kazi yake kutokana na uwezo aliokupa. Tunaona tena hapa “naked eye” inavyoweza kuleta matokeo mazuri ama mabaya.
Daudi+
Goliathi+
Majeshi ya Israeli+
Majeshi ya Wafilisti+
Majeshi ya Maadui yatakuja kwa njia moja baada ya “timbwili” yatatoka nduki kwa njia saba. Katika safari ndefu ya KUMJUA MUNGU kuna mengi yaumizayo lakini hupaswi KUKATA TAMAA.
Wafilipi 3:7
Inahitaji muda wa ziada katika kuutafuta uso wake ili kufikia UKAMILIFU (dhambi haitapata nafasi)
Imba wimbo huu
“More About Jesus R 432”
Nyimbo za Injili Na. 59
“Nizidi Yesu Kumjua”
Stanza 1.
Nizidi Yesu kumjua,
Mapenzi yake kufanya,
Na nizidi kuzijua
Pendo na wokovu pia
Chorus:
Zaidi ya Yesu,
Zaidi ya Yesu,
Nizidi kumjua sana
Pendo na wokovu pia.
















Imetayarishwa na Jabir Johnson, Septemba 7, 2014 

Post a Comment

0 Comments