KUOKOKA NI KUBADILIKA ASEMA MCHUNGAJI MWAKITALU

Kukiwa tulivu ndani ya kanisa la Tanzania Assemblies of God Ilomba Jijini Mbeya majira ya saa 3:00 asubuhi ya Jumapili ya Februari 5 Mtumishi wa Bwana Mchungaji na Mwalimu Vinac Amnon Mwakitalu anasimama na kuitaka hadhira ya waamini wa Kanisa hilo kutambua kuwa Yesu anamtafuta mtu anayemtafuta.
 MCHUNGAJI VINAC AMNON MWAKITALU
Akizungumza kwa msisitizo katika ibada hiyo ya kwanza Mchungaji Mwakitalu alisema Yesu anakuwa rafiki wa Zakayo kwasababu Zakayo alidiriki kumtafuta Yesu.

Katika mahubiri yake yaliyokuwa na kichwa kisemacho “KUOKOKA NI KUBADILIKA” alinukuru maandiko kwenye Biblia Takatifu Luka 19:1-10 na kusema Zakayo hakuwa rafiki wa jamii aliyokuwa nayo kutokana na sifa ya watoza ushuru.

Mchungaji Mwakitalu aliongeza  kusema watoza ushuru walichukiwa na jamii kutokana na tabia yao ya wezi, wakatili, waasherati, wenye kujipendekeza kwa watawala hivyo Zakayo mpaka anamtafuta Yesu alikuwa katika uhitaji na nafsi yake.

Pia Mchungaji Mwakitalu alisema kuokoka ni kubadilika ndani ya Kristo na kuwataka wajichunguze kama wanabadiliko ndani ya Kristo na kwamba hali zote mbaya mtu akishaokoka huondoka.

Aidha Mchungaji Mwakitalu alisema mabadiliko ya mwamini huja kwa kusoma na kujifunza Neno la Mungu na kufanya maombi.

CHANZO: JAIZMELALEO

Post a Comment

0 Comments