Mchungaji Kanyumi akemia migogoro makanisani

Mwinjilisti Genoveva Mikomanga, akionyesha kiapo.
Makamu Mkuu wa Askofu wa Kanisa la African Inland Church Tanzania (AICT), Dayosisi ya Mwanza  Mchg Henry Kanyumi, amewataka Watumishi wa Mungu kuendelea kuimarisha amani ya nchi na siyo kuleta migogoro ndani ya makanisa.


Mchg Kanyumi  aliyasema hayo Jumapili Novemba 11, 2019 wakati wa Ibada  maalum  ya kumweka wakfu na kusimikwa kazini, Mwinjilisti Genoveva Mikomanga,  kuwa  mtumishi katika Kanisa jipya la AICT Mlima wa Mizeituni katika ibada maalumu ambayo ilifanyika Makao Mkao Makuu ya (AICT) Makongoro  Jijini Mwanza wengine waliowekwa wakfu na kusimikwa kazini ni Wazee sita wa kanisa hilo hafla ambayo iliyoongozwa na Makamu Askofu Mkuu wa kanisa hilo nchini.

Mchg  Kanyumi alisema katika ulimwengu tuliopo sasa, migogoro imejaa na sasa inaonekana kama kitu chema na cha kawaida na migogoro hiyo  inayoanzia katika familia, jumuia, vijiji, wilaya, mikoa na hata  katika taifa letu kwa jumla.

Makamu Askofu Mchg Kanyumi akinukuu kitabu cha Waebrania 13:17 “Watiini wenye kuwaongoza na kuwanyenyekea ambapo  aliwaagiza wazee wa kanisa kumtii Mwinjilisti, na kwamba wasimame  katika kusheshimiana na kunyenyekeana.

“Ipo migogoro mingine baina ya ndugu na ndugu, jirani na jirani na hata pengine ya kabila na kabila, licha ya ile ya kimataifa,  ipo pia migogoro ya kidini yaani kutokuelewana kati ya Mchungaji na Wazee wa kanisa, Mwinjilisti na wazee  unakuta hawaelewani, madhehebu ya kidini na miongoni mwa waamini wenyewe kwa wenyewe na migogoro  hiyo husababishwa na tamaa ya mali na madaraka, ubinafsi na chuki,”alisema Makamu Askofu Kanyumi.

Alisema hivi leo kuna familia ambazo haziwezi kukaa pamoja na kumaliza matatizo yao na badala yake huchukua njia za vita, ugomvi na hata pengine mauaji kama suluhisho la migogoro yao, na hiyo  yote inatokana na familia hizo kutokuwa na nafasi ya kukaa pamoja na kuzungumza, watu wanaishi katika ulimwengu wa kuoneana mashaka na hivyo baadaye kuishia katika fujo.


Akizungumza mara baada ya kuwekwa wakfu Mwinjilisti Genoveva Mikomangwa, alisema  anamshukuru Mungu hapa alipofika maana nilianza na kanisa lenye watu 55 hadi sasa ndani ya miezi mine ana zaidi ya waumini 400.

“Matarajio yangu ni kuona kanisa la Mungu linaongezeka, linakuwa na kukomaa, hata Bwana Yesu aliwahubiri watu 3,000 na waliweza kuokoka,  hivyo  natamani kuliona kanisa la Mungu,  si tu ongozeko la wingi wa watu bali kuona kanisa la Mungu linakomaa, natamani sana kuendelea kuwafungua wengine waliofungwa katika utumishi wa Mungu alionipa natamani kusimama kama mtumishi Deborah, liko kusudi kwani dunia bado ipo gizani,”alisema Mwinjilisti Mikomangwa.

Post a Comment

0 Comments