Kwanini siku zote tunabishana?



Ni Jumatano jioni, Rachel mwenye umri wa miaka 17, amemaliza kazi zake za nyumbani naye anataka kupumzika!

Anawasha runinga na kuketi kwenye kiti anachopenda.

Wakati huohuo, mama yake anaingia, naye hana furaha.

“Rachel! Kwanini unapoteza wakati ukitazama runinga badala ya kumsaidia dada yako kufanya kazi za shule? Hufanyi kamwe unachoambiwa!”

“Umeanza tena,” Rachel asema kimyakimya Mama akamkaribia,
 “Unasema nini?”

“Hakuna,” Rachel anasema akishusha pumzi, akizungusha macho kwa dhihaka.
Sasa mama amekasirika kwelikweli. “Hutazungumza name kwa njia hiyo!”
“Na wewe je?” Rachel amjibu.

Mapumziko kwisha...ubishi mwingine umeanza.

Rachel anaongeza kuni kwenye moto kwa njia tatu, unaweza kutambua njia hizo? Umewahi kujionea kisa kama hicho? Je wew na wazazi wako mnabishana kila wakati. Ikiwa ndivyo, nini chanzo na suluhisho la changamoto hiyo?

Post a Comment

0 Comments