WATOTO YATIMA WATAKIWA KUTOVUNJIKA MOYO


WATOTO Yatima waliopo katika kanisa wametakiwa kutovunjika moyo kkwani Yesu waliye naye ndiye mkuu na anaweza kuwasaidia.
Wakifundisha katika Darasa la Watoto katika Kanisa la Tanzania Assemblies of God Ilomba Mbeya Walimu Costan Mwenga na Samwel Moses walisema watoto wengi katika kanisa wameonekana kukata tamaa na maisha bila kutambua kuwa wanaye Baba aliyewaumba.
Aidha walimu hao waliwataka watoto yatima kujenga maisha yao kwa Kristo Yesu kwani baada ya yote hapa ulimwenguni watakwenda mbinguni wasipozimia mioyo.

Post a Comment

0 Comments