Na Johnson Jabir
MBEYA-TZ


Aliongeza kusema wengi huanzisha vitu pasipo kufanya tafiti na hujikuta wakiangukia pua na kile kitu walichoanzisha kutoendelea kabisa, hivyo yeye huheshimu sana watu wanaofanya tafiti katika vitu mbalimbali maana huja na majibu yaliyo sahihi.
Pia alisema mkoa wa Mbeya ni mkoa wa Wakristo hivyo ni vizuri wakapata ladha zinazoendana na mambo wanayoyafanya ikiwemo kupata habari mbalimbali kuhusu Mungu kupitia Magazeti ya Kikristo ya hapa nchini.
Hayo yamekuja kufuatia utafiti na ubunifu wa wanahabari wa Redio MbeyaFM kuona mbali namna gani watawafikia wasikilizaji wake, hivyo kipindi cha NURU ya JUMAPILI ambacho hurushwa siku ya Jumapili kila juma kuanzia saa 12:00 -3:00 Asubuhi kimepewa hadhi ya kusimamia usomaji wa magazeti hayo kuanzia saa 1;00 – 1:15 Asubuhi kila Jumapili ya juma.