IBADA YA JUMAPILI FEB 26: ILOMBA CHRISTIAN CENTRE MBEYA

KANISA la Tanzania Assemblies of God Ilomba Christian Centre Mbeya lilifanya Ibada iliyojawa na nguvu za Roho Mtakatifu ikifuatiwa na Meza ya Bwana (HOLY COMMUNION).
 MCHUNGAJI PETER LYAKURWA
Mhubiri wa Neno la Mungu alikuwa Mchungaji Peter Lyakurwa kutoka Chuo cha Biblia Itende Jijini Mbeya ambaye alihuburi kwa kina kuhusu ROHO MTAKATIFU na kazi zake na kuongeza kuwa miongoni mwa dhambi ambazo mwamini hataweza kusamehewa ni kumkufuru Roho Mtakatifu.

Mchungaji Lyakurwa aliweka bayana  kuhusu uwepo wa Yesu katika kila kazi aifanyayo Roho Mtakatifu kwamba Yesu hulithibitisha Neno lake na kuongeza kuwa ni haki ya kila mwamini kujazwa na Roho Mtakatifu.






 MCHUNGAJI PETER LYAKURWA AKIHUBIRI KANISANI ILOMBA MBEYA KWA MCHUNGAJI VINAC AMNON MWAKITALU

Post a Comment

0 Comments