MILIONI 3 KUTOLEWA SEMINA YA PASAKA ILOMBA MBEYA

ZAIDI ya shilingi milioni 3 zimetolewa kama ahadi kwa ajili ya kufanikisha semina ya Pasaka itakayojiri miezi michache ijayo katika Kanisa la Tanzania Assemblies of God Ilomba Jijini Mbeya.
 MWANAJEOLOJIA WA BONDE LA ZIWA NYASA WITGARD D. NKONDOLA
Changizo hilo limefanywa jana Jumapili katika Ibada maalum kanisani hapo na Mtumishi wa Bwana Mwanajeolojia wa Bonde la Ziwa Nyasa Witgard Daniel Nkondola.

Katika ibada hiyo maalum ya changizo ilitanguliwa na utambulisho uliofanywa na Mchungaji wa Kanisa hilo Vinac Amnon Mwakitalu.

Nkondola aliweka bayana kuwa mwamini ili aweze kula sahani moja na Yesu sharti awe Mtoaji na hakuna njia ya mkato katika hilo.

Aliongeza kusema kumjaribu Bwana Mungu ni kwa njia ya kutoa na kwamba utoaji lazima ufanyike kwa uaminifu na utoaji mzuri ni ule unatoa kitu kilicho bora.

Hata hivyo alisema waamini wa siku za leo wamekubali kutoa lakini sio vyote wanavyoweza kutoa hasa inapofikia wakati wa kutoa fedha na mali zao.

Semina ya Pasaka inatarajiwa kugharimu kiasi cha shilingi 3,040,000/=

Imeandikwa na Johnson Jabir, Mbeya

Post a Comment

0 Comments