Yesu wa Nazareti aliyekataa kufungamana na dini.

Masia mwana wa Mungu, kama Wakristo wanavyomwita anabakia kuwa mwalimu pekee anayenukuliwa kwa sasa kuliko mwalimu mwingine yeyote. Mafundisho yake yanakataa kujiweka katika dini fulani zaidi sana yakigusa moyo wa  mwanadamu na kuleta matokeo. Hakuna kama yeye.

KILA mwaka wakati kama huu huibuka wimbi kubwa la watu wanaoamini katika nadharia na wengine wanaomkashifu kwa kutumia njia mbalimbali kuhusu Yesu wa Nazareti (K.K 4 – B.K 30–33) aliyekufa msalabani kwa kile kinachoamini dhambi za wanadamu.

Wengi wao hujitahidi kwa nguvu zote kutafuta wapi kuliko na mashimo kuhusu Yesu Mnazorayo (Yesu wa Nazareti).

Unamfahamu msanii wa  Marekani Douglas Blanchard?

Douglas Blanchard ni nani?
Blanchard hufundisha masomo ya sanaa ya kuchora katika Chuo cha Bronx Community  kilichopo katika Chuo Kikuu cha New York.

Mkufunzi huyu huchora michoro kuhusu Yesu ambayo ina mtazamo wa kishoga (watu wanaofanya mapenzi ya jinsia moja).

Aidha Blanchard hutumia  uzoefu wake katika fani hiyo akijikita kwenye historia, elimu ya zamani kuhusu visasili na matukio ya sasa.

Alizaliwa katika jimbo la Dallas nchini humo, alitunukiwa Shahada ya Sanaa ya Uchoraji (BFA) na Chuo cha Kansas City mwaka 1981.

Pia alitunukiwa uzamili katika sanaa na Chuko Kikuu cha Washington mjini St. Louis mwaka 1986 na mwaka 1993 alitunukiwa MFA na Chuo cha Sanaa cha New York Academy.
Anamiliki studio yake ya uchoraji mjini Manhattan ya chini upande wa Mashariki.

Aidha alithibitishwa kuwa muumini wa Anglikana (Episcopal) katika ngazi ya Uaskofu mwaka 1982.

Blanchard alijipambanua kuwa mtu asiye na habari na Mungu na wala hawezi kuzijua.

Mwaka 2004 alifanya uzinduzi wa makumbusho yake kuhusu sanaa ya ushoga na usagaji jijini New York na mwaka 2007 alizindua katika mji wa Taos, New Mexico.

Haikutosha katika uzinduzi huo Blanchard alifanikiwa kuiweka hewani michoro yake katika ‘collection’ moja iitwaayo ‘The Passion of Christ: A Gay Vision’ yaani Mateso ya Kristo katika mtazamo wa kishoga.

Huyo ndiye Douglas Blanchard.

Makusudi ya makala haya ni kutaka kumweleza Yesu katika mtazamo wa asiyefungamana na dini yoyote, kwa lugha rahisi dini nyingine zina mtazamo gani kuhusu Masia huyo.

Mhadhiri wa Chuo Kikuu cha Oxford, England katika somo ya Kihindi, Shaunaka Rishi Das alikaririwa akisema,

“Ni vigumu sana kwetu kumweka Yesu huyu mpendwa wa Mungu katika kundi la Mkristo au Myahudi. Kwani alikuwa akizungumza kuhusu Baba yake tu na hakujiingiza katika siasa, dini au utajiri. Huduma kwa Mungu yalikuwa ni maisha yake, mapenzi yake na dini yake.”

Yesu pekee anabaki kuwa anayezungumzwa na kunukuriwa kuliko mwalimu mwingine yeyote hapa ulimwenguni.

Mafundisho yake yamekuwa yakigusa moja kwa moja moyo wa binadamu, hii imesababisha kuwa Yesu kuwa kipekee bila kuegemea upande wowote wa dini zote hapa duniani.

Mwandishi wa habari wa karne ya 20 Gilbert K. Chesterton (1874-1936) aliegemea katika mtazamo kwamba Yesu amekuwa akionyesha uwezo wake katika vipindi tofauti, mila na desturi tofauti na dini tofauti.

G.K Chesterton kama alivyokuwa akifahamika na wengi alienda mbali zaidi kwa kusema wakati Yesu akija duniani aliukuta utumwa wa hali ya juu katika maisha ya binadamu, lakini alijitahidi kuifanya dunia iamini kuwa ulimwengu unaweza kuwapo bila utumwa.

Katika makala haya tunajiuliza Yesu alikuwa wa dini gani?

Rish Das anatuachia maswali mengi katika kipindi hiki cha Pasaka,” Je, Wahindu wanaweza kumfuata Yesu? Je Wahindu wanaweza kumpenda Mungu kwa moyo na nafsi zao? Je unapaswa kuwa Mkristo ili umfuate Yesu? Sasa nani ni wa Yesu?

Imetayarishwa na Jabir Johnson........Machi 27, 2016

Post a Comment

0 Comments