Kuna ulazima wa kuliinua na kuliheshimisha kanisa (mahali pa kuabudia)?

1. Umewahi kukutana na mtoto anayependa baba amtumie "pocket money" lakini kimsingi hampendi baba yake? Umewahi kufikiri siku baba yake akimwambia sina hela itakuwaje?

2. Umewahi kukutana na waziri mchapa kazi, mwenye ustadi wa hali ya juu, anayependwa na watu kiasi kwamba wako tayari walale chini yeye apite awakanyage juu, na kwasababu hiyo kawafanya watu hao hao wasiwe na mpango na Rais aliyempa mamlaka akiwaaminisha watu yeye ndio jibu lao? Umewahi kufikiri maumivu ya Rais aliyonayo?
 
3. Hivi umewahi kujiuliza kati ya glass na maji kipi ni muhimu zaidi? 
 
Hizi ni Kansa Hatari Sana kwa kanisa la leo...
1. Kupenda baraka kuliko kumpenda mtoa baraka
2. Kumtukuza mtumishi kuliko kumtukuza Mungu
3. Kuliinua na kuliheshimisha kanisa (mahali pa kuabudia) kuliko kumuinua na kumheshimisha Mungu
NB: Pamoja na kwamba tuliambiwa tuwe na imani, lakini hatukuambiwa tuziweke akili pembeni 

Mtoaji wa Neno la Hekima: Paul Francis Masele

Post a Comment

0 Comments