TAG kuadhimisha miaka 80 tangu kuanzishwa kwake

Mchungaji Benjamin Bukuku wa Kanisa la Tanzania Assemblies of God-Soweto, Moshi.


Kanisa la Tanzania Assembles Of God (TAG), linatarajiwa kuadhimisha maadhimisho ya  kutimiza miaka 80,  tangu kuanzishwa kwake mwaka 1939 ambapo maadhimisho hayo yatafanyika Jimbo la TAG Amani Soweto mjini Moshi mkoani Kilimanjaro Mei 26 mwaka huu.
Akizungumza na waandishi wa habari ofisini kwake Askofu Mkuu wa kanisa hilo, Jimbo la Kilimanjaro Magharibi ambaye pia ni Mchungaji Kiongozi wa kanisa la Amani Soweto, Dkt Benjamin William Bukuku alisema katika maadhisho hayo ambayo yatatanguliwa na matembezi ya amani yataanzia katika kanisala la International Christian Cente (KICC) la mjini Moshi hadi Jimboni  ambapo kanisa la TAG  lililopo  maeneo ya Soweto mjini Moshi mkoani hapa.
Alisema katika maadhimisho hayo mgeni rasmi anatarajiwa kuwa mkuu wa mkoa wa Kilimanjaro Dkt. Anna  Elisha Mghwira, pamoja na mgeni maalumu kutoka makao makuu ya TAG Jijini Dar es  Salaam Mchungaji  Moses  Magembe.
“Katika maadhimisho haya  tutakuwa na shughuli mbalimbali za kijamii  ambazo zitafanyika, moja wapo ni upandaji wa miti kuzunguka eneo letu  la Jimbo, ambapo zoezi hilo litafanywa na  Mkuu wa mkoa wa Kilimanjaro kwa kushirikiana  na  waumini wote,”alisema Askofu Dkt Bukuku.
Aidha Askofu  Dkt Bukuku, alisema katika maadhimisho hayo pia  waumini wa kanisa hilo, watatembelea katika gereza Kuu la Karanga, kwa ajili ya kutoa huduma za neno  la Mungu pamoja na kuwapatia misaada mbalimbali ya kijamii wafungwa walipo katika gereza hilo.
Hata hivyo Askofu Bukuku alisema kanisa linajivunia kutimiza miaka 80 ttoka kuanzishwa kwake na kwamba litaendelea kuhamasisha amani, umoja na mshikamano kwa kueneza injili kwa mataifa yote.
Maadhimisho hayo yatakwenda sanjari na  hitimisho la mpango mkakati wa miaka 10 ya mavuno  ambayo  kilele chake kitafanyika Julai Mwaka huu Jijini Arusha.
Kanisa la Tanzania Assembles Of God (TAG),  linatarajiwa kuadhimisha maadhimisho ya  kutimiza miaka 80,  Mei 26 mwaka ya tangu kuanzishwa kwake mwaka 1939 ambapo maadhimisho hayo yatafanyika Jimbo la TAG Amani Soweto mjini Moshi mkoani Kilimanjaro.
Pia katika maadhimisho hayo yatakwenda sanjari na  hitimisho la mpango mkakati wa miaka 10 ya mavuno  ambayo  kilele chake kitafanyika Julai Mwaka huu Jijini Arusha.
Hayo yamesemwa na Askofu Mkuu wa kanisa hilo, Jimbo la Kilimanjaro Magharibi ambaye pia ni Mchungaji Kiongozi wa kanisa la Amani Soweto, Dkt Benjamin William Bukuku, wakati alipokuwa akizungumza na waandishi wa habari ofisini kwake kuhusiana na maadhimisho hayo.
Askofu Dkt Bukuku alisema katika maadhisho hayo ambayo yatatanguliwa na matembezi ya amani yataanzia katika kanisala la International Christian Cente (KICC) la mjini Moshi hadi Jimboni  ambapo kanisa la TAG  lililopo  maeneo ya Soweto mjini Moshi mkoani hapa.
Alisema katika maadhimisho hayo mgeni rasmi anatarajiwa kuwa mkuu wa mkoa wa Kilimanjaro Dkt Anna  Elisha Mghwira, pamoja na mgeni maalumu kutoka makao makuu ya TAG Jijini Dar es  Salaam Mchungaji  Moses  Magembe.
“Katika maadhimisho haya  tutakuwa na shughuli mbalimbali za kijamii  ambazo zitafanyika, moja wapo ni upandaji wa miti kuzunguka eneo letu  la Jimbo, ambapo zoezi hilo litafanywa na  Mkuu wa mkoa wa Kilimanjaro kwa kushirikiana  na  waumini wote,”alisema Askofu Dkt Bukuku.
Aidha Askofu  Dkt Bukuku, alisema katika maadhimisho hayo pia  waumini wa kanisa hilo, watatembelea katika gereza Kuu la Karanga, kwa ajili ya kutoa huduma za neno  la Mungu pamoja na kuwapatia misaada mbalimbali ya kijamii wafungwa walipo katika gereza hilo.
Hata hivyo Askofu Bukuku alisema kanisa linajivunia kutimiza miaka 80 ttoka kuanzishwa kawake na kwamba litaendelea kuhamasisha amani, umoja na mshikamano kwa kueneza injili kwa mataifa yote.
STORY BY: Kija Elias


Post a Comment

0 Comments