TAG Soweto yazuru gereza la Karanga, Moshi


Makamu  Askofu  Mkuu  wa Kanisa la Assembles Of God  (TAG), Jimbo la Kilimanjaro Magharibi, Mchungaji  Allen  Lekei amewataka wafungwa walioko magerezani kujiweka mikononi mwa Mungu siku zote za maisha yao ili kuepukana na changamoto za kuwa mbali na Mungu.

Askofu Lekei aliyasema hayo wakati walipotembelea wafungwa katika gereza Kuu  la Karanga la Moshi na ikiwa ni maadhimisho ya  kutimiza miaka 80 pamoja na mpango mkakati wa miaka 10 ya mavuno ya (TAG), ambapo waliwalisha neno la Mungu pamoja na kutoa misaada mbalimbali ya kijamii yenye thamani ya  shilingi laki  7.
Mchungaji Allen Lekei, alisema  liko tumaini kwa Mungu kwa watu waliovunjika moyo, waliokata tamaa, kwani hapo sio mwisho, kwani kukaa mbali na Mungu  kuna changamoto nyingi.
Aliwaasa kwa kuwatia moyo kuwa maisha  wanayoishi kwa sasa yasiwafanye kukata tamaa, kwani  ipo siku Mungu atawwaonea huruma  hata wahukumu kwa dhambi zako. 
Aidha aliwatia moyo kwa kuwasihi kuwa toba ina nguvu, ina marejesho kwa Mungu, hivyo aliwaomba waendelee kuvaa mavazi ya  wokovu, mavazi ya upendo.
Akitoa nenoo la shukurani kwa niaba ya wafungwa wenzake Mnyampara Mkuu wa gereza la wanawake Karanga, Sofia Kingazi, aliwaomba kuendelea kuja na  kutoa neno la Mungu.
“Tunashukuru mno kwa kuja na kutuona, kubwa zaidi tumefarijika sana na ujumbe wa neno la Mungu, hivyo tunaomba  msiishie kuja leo tu kwa ajili ya kutulisha neno la Kiroho,”alisema Kingazi.
Kwa upande wake Mkurugenzi mstaafu wa Wanawake watumishi Wakristo (WWK) Tanzania ambaye pia ni Mchungaji Kanisa la (TAG ) Chekereni Lidia Materu, alisema kama unapita kwenye kipindi kigumu  Mungu  anasema usiogope.
“Mungu  ametupa agizo la kuwaona  watu waliofungwa, wagonjwa yatima na watoto yatima, hivyo ni vizuri kuwaona watu wenye uhitaji watu  wakipatanishwa na Mungu watajisikia kumtumainia Mungu  kuliko kutumia akili zao kwa mambo ambayo hayatawezekana,”alisema Mchungaji  Materu.
Mchungaji Materu  aliongeza kusema kuwa “Ikiwa umeshindwa kuulinda moyo wako kwa sababu ya kuzidiwa na  mambo magumu na mabaya , usikate tamaa, bado tumaini lipo,  wengi hudhani kwamba  upako wa Roho mtakatifu ni kwa ajili ya kuhubiri habari njema na kuombea wagonjwa tu, lakini neno la Mungu  linaonyesha  wazi  kwamba kuna upako wa kuganga mioyo iliyovunjika,”alisema.

Post a Comment

0 Comments