Theolojia: Mwanamume na Mwanamke wa Kwanza




Zaburi 83: 18; Mwanzo 1:26-31; 2:7-25: Unaona tofauti gani katika uumbaji wa binadamu. Mwanamume na mwanamke wa kwanza. Nani aliwaumba? Ni Mungu. Unajua jina lake? Ni Yehova. 


Mwanamume na mwanamke waliitwa Adamu na Hawa. Yehova Mungu aliumba Adamu hivi. Alichukua mavumbi akafanya mwili mzuri wa mwanamume. Kisha akapuliza katika pua, Adamu akawa hai. Yehova Mungu alimpa Adamu kazi ya kuwapa wanyama wote majina. 


Labda Adamu aliwatazama wanyama muda mrefu ili aweze kuwachagulia majina bora. Adamu alipokuwa akiwa wanyama majina aliona jambo fulani. Unajua ni jambo gani?



Wanyama wote walikuwa na wenzao. Tembo baba na mama walikuwapo, hata samba baba na mama walikuwapo. Lakini Adamu hakuwa na mwenzake. Basi Yehova  akampa Adamu usingizi mzito, akachukua ubavu wake mmoja. 

Kwa ubavu huo, Yehova alimfanyia Adamu mke. Adamu akafurahi! Wazia Hawa alivyofurahi alipowekwa katika bustani hiyo nzuri! Wangeweza kuzaa watoto wakae pamoja kwa furaha. 

Yehova alitaka Adamu na Hawa wakae milele. Alitaka waifanye dunia nzima iwe nzuri kama bustani hii ya Edeni. Adamu na Hawa walifurahia sana hilo. Wewe ungependa kuifanya dunia iwe bustani nzuri? 

Lakini furaha ya Adamu na Hawa haikuendelea. Kwanini haikuendelea. Zaburi 83: 18; Mwanzo 1:26-31; 2:7-25:

Post a Comment

0 Comments