MKUU WA WILAYA ALITAKA KAMPUNI LA UNUNUZI WA KAHAWA KUACHA KUTUMIA JINA LA YESU


Mkuu wa Wilaya ya Mbeya Evans Balama amelikemea kampuni la Ununuzi wa Kahawa Wilayani Mbozi mkoani Mbeya (LIMA Ltd) kuacha tabia ya kulitumia JINA LA YESU kulaghai wakulima wa zao hilo.
Akizungumza katika mkutano wa Wadau siku chache zilizopita Balama alisema Uongozi wa Kampuni hilo umekuwa ukijifanya kumjua Mungu sana huku likiwaibia wananchi na wakulima wa kahawa wilayani humo.

Balama aliongeza kusema kulitumia Jina la Yesu visivyo ni kumuonea Yesu na ukuu aliokuwa nao kwani katika huduma yake hakuwahi kumlaghai mtu yeyote katika Israeli na vitabu vingi vinathibitisha ukuu na upekee wake.

Pia aliongeza kusema Kampuni hilo halitakiwa kutumia mwavuli wa dini kujinufaisha huku likijua ni kosa kisheria kufanya  hivyo.

Mbali ni hilo aliweka bayana kuhusu kampuni hilo limekuwa likinunua kahawa mbichi kinyume cha sheria ya zao hilo ya mwaka 2001 inayotaka kahawa inunuliwe kwa kuzingatia madaraja yaliyopangwa katika sheria hiyo.

Balama aliongeza kusema kahawa mbichi sio sahihi kabisa kununuliwa kwani inapunguza ubora wa zao hilo katika soka la dunia na kuwaacha wananchi na wakulima wa zao hilo katika hali ya umaskini.

Katika mkutano huo wa wadau uliosimamiwa na Mkuu wa Wilaya ya Mbozi Gabriel Kimolo huku mgeni rasmi akiwa  Profesa Jumanne Maghembe ambaye ni Waziri wa Kilimo, Chakula na Ushirika hapa nchini.

Zao la kahawa kabla ya mwaka 2007 lilikuwa chini nchini Tanzania lakini kwa sasa bei yake ipo juu hivyo kuuza kahawa mbichi ni kumuone mkulima wa zao hilo na katika mmkoa wa Mbeya Mashamba makubwa yapo Lunji, Utengule na Mpunguluma(Mbeya Vijijini), Mbimba, Msumbi, Kanji Lalji, Shiwanda, Kamaro, Elton (Mbozi ) na mkoa Mbeya una jumla ya hekta 156, 420 za zao hilo.

Post a Comment

0 Comments