KIKWETE KADHALILISHWA

YAH: KUDHALILISHWA KWA RAIS KIKWETE KWENYE  FACEBOOK
Blogu ya JAIZMELALEO ikishirikiana na blogu ya MCRCTV kwa pamoja tunapenda kutoa msimamo wetu katika suala hili la matumizi ya mtandao.

Katika ukurasa wa facebook kuna picha mabayo si haki na ni kitendo cha aibu kwa Mkuu wa nchi ya Tanzania Mheshimiwa Rais Jakaya Kikwete kuonyeshwa katika vazi la kikahaba.

Yapo matukio mengi ya viongozi wengi ulimwenguni wanaofanyiwa hivyo lakini kwa kuona umuhimu kwa taifa na watumiaji wa mitandao ya kijami kilichofanyika hapo sio haki hata kama ni uhuru basi umepitiliza.

Anuani hiyo imeandikwa “FISADI KIKWETE” kutoka Dar es Salaam Tanzania ambayo katika profile picture imewekwa picha hiyo bofya linki hii.

TUNASEMA hii ni kashfa hatua za makusudi lazima zichukuliwe kwa mtu au kundi la watu wanaojihusisha na tabia hizi za udhalilishaji kwa kiongozi mkubwa kama huyu mwenye heshima nchini Tanzania.

Licha ya kwamba kwa upande wake kama Rais anatakiwa aichukue kama changamoto ili kujipanga vizuri, kujichunguza nyendo zake bila hivyo zitazidi zaidi ya hapo.

TUNAWAOMBA watanzania waheshimu maadili ya mtanzania hata kama kuna makosa kwa mtu husika lakini taratibu zipo na zichukuliwe.
UONGOZI WA BLOGU ZA JAIZMELALEO NA MCRCTV
Januari 20, 2012

Post a Comment

0 Comments